Kila Tiba kati ya zifuatazo ni yenye kujitegemea.Chagua iliyo rahisi kwako.Isipokufaa ndipo uchague nyengine.
TIBA A:
Tafuta:vijiko(10ml) 2 vya chakula vya udi karaha,vijiko(10ml) 2 vya habat souda,vijiko(10ml) 2 vya mbegu za figili,vijiko(10ml) 2 vya filfil-ab-yabwi,vijiko(10ml) 2 vya basbasi jauzi,vijiko(10ml) 2 vya tangawizi,vijiko(10ml) 2 vya karafuu, vijiko (10ml) 2 vya Darufil-fil,vijiko(10ml) 2 vya khulinjani,Nusu (1/2) lita ya asali.
  Kipimo cha kila dawa ni lazima iliyotwangwa.
  Baada ya kuchanganywa na asali tumia kijiko kimoja (5ml) cha chai kutwa mara tatu (1×3) kwa muda wa siku (15-21).
TIBA B: HAL-WATU THAUM
Tafuta:Kilo 1 ya nyama ya mbuzi iliyosagwa,Chupa (750ml) ya maziwa ya Ng’ombe,Nusu lita (500ml) ya asali,Lita moja na robo (1250ml) ya samli safi,Kilo 1 ya vitunguu thaumu,1/2 kilo ya ufuta,1/2 kilo ya tende.
 Changanya madawa yote halafu pika mpaka iwe kama ugali .
Tumia kijiko 1 (10ml)  kutwa mara tatu (1×3) mpaka dawa yote ishe.
TIBA C: KHULINJANI
Tafuta khulinjani na itwange.Changanya na asali kijiko 1 (10ml) .
 Tumia kijiko kimoja cha chai (5ml) unywe na maziwa gilasi 1 kutwa mara tatu (1×3) kwa muda wa siku (15-21)Â
 TIBA D:
  Tafuta asali vijiko 2 vya ckakula (10ml),Tende kokwa 7,Kijiko cha chai (5ml) cha mbegu za habbat saudai,Mafuta ya habbat saudai kijiko 1 cha chai (5ml) na mbegu 40 za Lozi.
  Changanya madawa haya na kunywa glasi moja (250ml),rudia kutwa mara tatu (1×3) kwa siku (15-21).
 TIBA E:
 Tafuta 100grm za tangawizi mbichi,20grm za pipili manga na punje 25 za vutunguu thaumu.Twanga dawa hizo Tayarisha supu ya pweza robo kilo (1/4kg),Changanya madawa hayo na supu ya pweza .
 Tumia kila siku jioni kwa muda wa siku (15-21)
About Author

Advertisement

Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment